+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Alhamisi, 16 Julai 2015

MAMBO MAWILI(2) MUHIMU ILI KUPEWA KIBALI CHA KUJENGA JENGO



Habari za wakati mpendwa msomaji! hivi kwa kawaida ni watu wangapi ambao wanafikiria kujenga? hapana shaka ukifanya utafiti utakuta kila binadamu mwenye akili timamu anafikiria kujenga. Hivyo basi twende pamoja katika habari hii muhimu kwako.
Kabla ya yote bonyeza maandishi ya bluu hapo chini ili kusoma habari zilizokwisha wekwa ambazo zinaweza kukusaidia
vitu vya kuchunguza kabla hujanunua kiwanja
Kabla hujafikiria kujenga zingatia haya
Vitu 11 vya kuzingatia katika michoro ya jengo ili kupata kibali
Hatua za kufuata ili kupewa kibali cha kujenga jengo.
   Kwanza kabisa wanaotoa kibali cha kuruhusu jengo lijengwe  ni mamlaka za kiserikali za eneo husika hasa manispaa, kwa maana wao wanao ramani ya mji mzima inayoonesha mipangilio ya aina za majengo yanayotakiwa kujengwa katika kila mtaa.
1. Hati halali ya eneo – Hii hasa kwa wale wanaotaka kujenga majengo ya gholofa na ya kibiashara ni lazima kuhakikisha unakuwa na hati halali inayoonesha kwamba sehemu unayotaka kujenga ni mali yako.

mfano wa hati ya kiwanja
2. Michoro kamili na iliyowekwa muhuri – hii ni ile ya msanifu majengo(architectural drawings) kwa majengo ya kawaida ya kuishi(residential) ya chini (one storey) kwa yale ya ghorofa pia itahitajika michoro ya mhandisi majengo(structural drawings), mhandisi umeme (electrical drawings), na michoro ya mfumo wa maji safi na taka (plumbing).

mfano wa ramani ya muonekano wa jengo (3dimension)

 
Kumbuka : michoro hii yote inatakiwa iwe imepigwa muhuri ili kuonesha kwamba imechorwa na wataalamu wenye sifa na wanaotambulika.
kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965
usiache kuweka neno hapo chini

1 COMMENT

EMMANUEL REUBEN alisema ...
23 Septemba 2020, 01:26

HABARI MIMI NIMEKUTANA NA CHANGAMOTO MOJA -KIWAJA CHANGU NIMEPIMA NASUBIRI HATI,NIKAANZA UJENZI NIKASIMAMISHWA NA MTU FULANI AKANIAMBIA SINA KIBALI CHA KUJENGA ,AKANIAMBIA ANATOKEA KWA MWENYEKI MTENDAJI WA MTAA,HIVYO NIFIKE CHA AJABU WAKANIAMBIA NILIPE KIASI FULANI BILA KUPEWA CHOCHOTE CHA UTHIBITISHO KWA AHADIYA KULINDWA HADI NIMALIZE UJENZI,NIKATOA NUSU LAKINI NINA WASIWASI SANA KAMA NI NJE YA UTARATIBU,NA KWA MUJIBU WA MAELEZO YENU MIMI BADO SINA HATI NA NAHITAJI KUENEDELEA NA UJENZI KIDOGO KIDOGO WA NYUMBA YA KUISHI YA ROOM 3,JE NIFANYEJE ILI KUPATA LIBALI HALALI-0714-49-31-51 NAMBA YANGU KWA MSAADA ZAIDI,


Chapisha Maoni

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506