+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Jumatatu, 13 Julai 2015

HISTORIA YA LEONARDO DA VINCI KATIKA UJENZI

 

image

Habari za wakati huu mpendwa msomaji wa makala hizi za ujenzi.

katika historia leo tunamuangalia mmoja kati ya watu waliokuwa wataalamu wa kuzaliwa katika maswala ya ujenzi (msanifu majengo).

Leonardo da vinci ni msanifu majengo, mwanasayansi, mwanamuziki, mchoraji, mchongaji, mhandisi, mwanamahesabu, mwana jiolojia, mwana atonomia, na mwana botania aliyezaliwa tarehe 15 mwezi wa 4 mwaka 1452 mji wa vinci nchi ya Italy na kufariki tarehe 2 mwezi wa 5 mwaka 1519 (akiwa na miaka 67) mji wa amboise nchi ya Ufaransa

Japo ni muda wa miaka 496 umepita sasa lakini bado kazi zake zimekuwa zikitumiwa na wanasayansi katika tafiti zao, pamoja na baadhi ya picha alizozitengeneza na kuuzwa kwa gharama kama ile ya mona lisa aliyoichora mnamo mwaka 1503-1505.

image

Katika teknolojia ya ujenzi leonardo da vinci alitumia muda wake kusoma uwiano wa mwili wa binadamu (human proportional) na kuchora mchoro unaoonesha uwiano huo mnamo mwaka 1492 ambayo inatumiwa na wasanifu majengo wanapokuwa wanaanza kubuni ukubwa wa jengo.

image

 Pia katika teknolojia ya ujenzi leonardo da vinci kupitia kazi zake pamoja na maelezo yake aliyokuwa akiyaandika kwa siri (yaani mpaka uweke kioo ndiyo yanasomeka), alichora picha kuonesha muonekano wa jengo kwa kutumia uwiano wa macho (3 dimension) mnamo mwaka 1490s ambazo zinatumiwa na wasanifu majengo mpaka sasa

image

Kazi nyingine alizozifanya leonardo da vinci

Taswira ya mwanamuziki mwaka 1490

image

Taswira ya madonna na mtoto mwaka 1470s

image

Taswira ya mwili wa mwanamke mwaka 1506-08

image

Taswira ya fuvu mwaka 1489

image

Mchoro wa mashine mwaka 1480

image

Mchoro wa mashine ya kupaa (flying machine) mwaka 1486-90

image

Na hii ni kazi iliyombebea umaarufu zaidi inaitwa “the last supper” mwaka 1495-98

image

SOURCE: LEONARDO DA VINCI FOR KIDS BOOK

Ni kazi nyingi alizozifanya Leonardo da vinci ila tunaishia hapo kwa sasa, kwa historia zake zingine na za wataalamu wengine wa zamani endelea kututembelea.

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia

email: ujenzielekezi04@gmail.com

Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

0 COMMENTS

Chapisha Maoni

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506