+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Jumamosi, 12 Septemba 2015

UWEKAJI (INSTALLATION) YA UMEME WA NYUMBANI KATIKA UJENZI



Habari za wakati mpendwa msomaji! tunatumaini umzima wa afya na unaendelea na majukumu yako ya kila siku.
Katika ujenzi kila kazi/kitu kina muda wake mfano huwezi peleka mabati kwenye eneo unalojenga(site) wakati ndiyo kwanza unachimba msingi hivyo basi hata mfumo wa umeme unamuda wake.
Kumbuka: Lengo la kukuwekea mada hii ni kukupa a,b,c.. wewe unayefikiria kujenga au umeshajenga sasa unataka kufanya marekebisho(maintenance).
Wakati wa kuanza kuweka mfumo wa umeme kwenye nyumba.
Baada ya mchoro wa umeme kukamilika (electrical drawing) unaoonesha jinsi mfumo wa umeme utakavyopita kwenye nyumba yako, mfumo huu unaanza kuwekwa katika ngazi zifuatazo;
Mfano wa mchoro wa umeme
  • Kabla ya kupiga lipu(plaster) – Huu ndiyo wakati wa awali kabisa wa kuanza kuweka mfumo wa umeme ambapo mafundi umeme hupitisha mabomba na vibox vya kuwekea switch,socket na distribution box (db).
Jinsi mabomba ya umeme yanavyopitishwa
  • baada ya kufanya umaliziaji(finishing) ya ukuta na kuweka ceiling/gypsum board – wakati huu ndiyo wa mwisho kumalizia kuweka(install) mfumo wa umeme ambapo mafundi umeme wanapitisha nyaya na kupachika taa, switch, socket, nk .
switch

Kumbuka: kama utaratibu huu hautafuatwa basi itabidi mafundi umeme watindue ili kupitisha mabomba wakati umeshafanya umaliziaji (finishing).

Kama upo dar-es-salaam au Dodoma na unashida ya kutatuliwa tatizo lolote linalohusu umeme kwenye nyumba unayojenga/uliyojenga tutafute kwa namba +255753066151 na tutakukutanisha na mafundi umeme wa uhakika

USIPITWE: Endelea kuwa nasi kwa taarifa hizi na nyingine kuhusu ujenzi. 

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

Alhamisi, 10 Septemba 2015

JE UNAFAHAMU WAKATI SAHIHI WA KUHAMIA KWENYE NYUMBA KAMA UNAJENGA KIDOGO KIDOGO?



Habari za wakati mpendwa msomaji! Karibu tena kwenye uwanja huru wa kujipatia taarifa na elimu mbadala kwa mambo ya ujenzi.
Ujenzi wa nyumba ya kuishi ni jukumu ambalo kila mtu hulifikiria pale anapofikisha umri fulani wa kujitambua, mara nyingi sio kila mtu anayefikiria hupata fursa ya utekelezaji la hasha hutegemea kipato cha mtu na bajeti yake na ndiyo maana nyumba hutofautiana pia katika ubunifu na malighafi(material) zitakazo tumika.
Kwa ufupi katika ujenzi wa nyumba ya kuishi kuna hatua nne za kuzingatia;
1. Msingi – hii ni hatua ya kwanza ya ujenzi wa nyumba baada ya kumaliza uchoraji wa ramani na upimaji wa kiwanja na nyumba itakavyokaa (setting out)

2. Upandishaji wa ukuta – hii ni hatua inayofuata baada ya msingi. angalia picha hapo chini

3. Uwezekaji


4. umaliziaji – hii ndiyo hatua ya mwisho na ndiyo hatua ambayo mtu anaweza kuhamia. hatua hii inavitu vingi sana hivyo basi ili uweze kuhamia itakubidi uhakikishe vitu vifuatavyo vya hatua hii umevikamilisha, madirisha, milango(sana sana ya kutokea nje), uwekaji wa mabomba kwa ajili ya umeme na maji, kusakafia(flooring) na kupiga lipu (plaster)

Kumbuka: Lengo la kukuwekea mada hii ni kukupa a,b,c.. wewe unayefikiria kujenga au umeshajenga sasa unataka kuhamia.
Bonyeza maandishi ya blue hapo chini kwa taarifa nyingine zinazoweza kukusaidia
vitu vya kuchunguza kabla hujanunua kiwanja

Kabla hujafikiria kujenga zingatia haya

Vitu 11 vya kuzingatia katika michoro ya jengo ili kupata kibali

USIPITWE!! Endelea kuwa nasi kwa taarifa nyingine kuhusu ujenzi.

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506