+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Jumatatu, 3 Novemba 2014

Hii ndiyo orodha ya watu wanaohusika kukamilisha kazi za ujenzi (building team)

   mpendwa msomaji wa makala hizi zinazohusu ujenzi, hapo chini utaona orodha ya watu wanaohusika na ujenzi kwanzia mwanzo mpaka mwisho pamoja na majukumu yao.

pic 1
1. Mteja/mwajiri
huyu ndio mtu au watu wa msingi katika ujenzi ambaye ndiye mhitaji wa jengo, mmiliki wa kiwanja, na mwezeshaji au mwekezaji wa jengo. mteja/mwajiri anaweza kuwa mtu, kikundi cha watu, idara, asasi, au serikali.
Mwajiri/mteja sio lazima awe na ufahamu wa maswala ya ujenzi
2. Timu ya wabunifu
Hawa ni watu wenye ujuzi wa ubunifu katika ujenzi wanaohusika na utengenezaji wa muonekano wa jengo na uandaaji wa mpango kazi. Timu ya wabunifu huwa na wabunifu wa aina tofauti kama msanifu majengo(architect), mkandarasi wa majengo( structural engineer) na wengineo. (tutawaelezea vizuri katika makala zijazo).
3. Msimamizi wa majengo(clerk of work)
Huyu ni mmoja wa wahusika katika timu ya ujenzi anayeajiliwa na mteja/mwajiri kwa lengo la kuhakikisha kwamba kontrakta (contractor) anajenga jengo kulingana na michoro ya jengo.
4. Timu ujenzi (construction team)
Hii ni timu inayowajibika kujenga jengo kulingana na mawazo na michoro kutoka kwa wabunifu kwa kuzingatia ubora, viwango, usalama, na uchumi uliopo. Timu hii pia inaunganisha watu wenye utaalamu tofauti tofauti kama mkadiriaji, mnyapara (foreman) na wengine wengi. (tutawaelezea vizuri kwenye makala zijazo).
5. Mgawaji/mletaji (supplier)
Huyu anahusika na kuleta/ kupeleka mahitaji kama cement, vigae, mchanga na vitu vingine vinavyohusu ujenzi eneo la ujenzi.
6. Mdhibiti/mrekebishaji (regulator)
Huyu anahusika na kulinda watumiaji wa jengo na wafanyakazi dhidi ya njia mbaya za ujenzi.
kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwenye email ujenzielekezi04@gmail.com
usisahau kuweka neno hapo chini

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506