+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Jumamosi, 12 Septemba 2015

UWEKAJI (INSTALLATION) YA UMEME WA NYUMBANI KATIKA UJENZI



Habari za wakati mpendwa msomaji! tunatumaini umzima wa afya na unaendelea na majukumu yako ya kila siku.
Katika ujenzi kila kazi/kitu kina muda wake mfano huwezi peleka mabati kwenye eneo unalojenga(site) wakati ndiyo kwanza unachimba msingi hivyo basi hata mfumo wa umeme unamuda wake.
Kumbuka: Lengo la kukuwekea mada hii ni kukupa a,b,c.. wewe unayefikiria kujenga au umeshajenga sasa unataka kufanya marekebisho(maintenance).
Wakati wa kuanza kuweka mfumo wa umeme kwenye nyumba.
Baada ya mchoro wa umeme kukamilika (electrical drawing) unaoonesha jinsi mfumo wa umeme utakavyopita kwenye nyumba yako, mfumo huu unaanza kuwekwa katika ngazi zifuatazo;
Mfano wa mchoro wa umeme
  • Kabla ya kupiga lipu(plaster) – Huu ndiyo wakati wa awali kabisa wa kuanza kuweka mfumo wa umeme ambapo mafundi umeme hupitisha mabomba na vibox vya kuwekea switch,socket na distribution box (db).
Jinsi mabomba ya umeme yanavyopitishwa
  • baada ya kufanya umaliziaji(finishing) ya ukuta na kuweka ceiling/gypsum board – wakati huu ndiyo wa mwisho kumalizia kuweka(install) mfumo wa umeme ambapo mafundi umeme wanapitisha nyaya na kupachika taa, switch, socket, nk .
switch

Kumbuka: kama utaratibu huu hautafuatwa basi itabidi mafundi umeme watindue ili kupitisha mabomba wakati umeshafanya umaliziaji (finishing).

Kama upo dar-es-salaam au Dodoma na unashida ya kutatuliwa tatizo lolote linalohusu umeme kwenye nyumba unayojenga/uliyojenga tutafute kwa namba +255753066151 na tutakukutanisha na mafundi umeme wa uhakika

USIPITWE: Endelea kuwa nasi kwa taarifa hizi na nyingine kuhusu ujenzi. 

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

2 COMMENTS

Bila jina alisema ...
23 Julai 2015, 21:45

nimewapata kwa hiyo a,b,c


Unknown alisema ...
17 Julai 2018, 23:46

hongereni sana kwa kazi nzuri mnazozifanya!


Chapisha Maoni

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506