+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo VIFAA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo VIFAA. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 25 Julai 2015

PICHA NA VITU VYA MSINGI KUWEPO KWENYE CHUMBA CHA KUPIKIA (KITCHEN)



Habari za wakati mpendwa msomaji! Karibu tena kwenye uwanja huru wa kujipatia taarifa na elimu mbadala kwa mambo ya ujenzi.

Mpendwa msomaji utaratibu wa kuweka chumba cha kupikia (kitchen) kwenye nyumba ya kuishi(residential) ulianza kuzingatiwa zaidi miaka ya 1920s na katika nchi zetu za kiafrika miaka ya 1970s japo mpaka sasa bado kuna baadhi ya maeneo haujazingatiwa. Utaratibu huu ulianzishwa hasa maeneo ya mijini kwa lengo la kupunguza matumizi ya eneo yasiyokuwa ya lazima na kwa ajili ya ulinzi(security and privacy).


Chumba cha kupikia(kitchen) ni chumba chenye pilika pilika (movement) nyingi karibia robo tatu siku (imekadiriwa kwamba mtu anayeandaa chakula kwenye chumba kisicho na mpangilio mzuri movement anazofanya ni sawa na mtu aliyetembea maili moja na nusu), hivyo basi ni vizuri kuweka mpangilio mzuri ili kupunguza pilika pilika(movement) zisizokuwa na msingi.

Kumbuka : wapo wataalamu waliobobea kwenye mambo ya upangiliaji wa ndani ya nyumba (interior designer) hivyo basi kama itakusumbua ni vizuri kumtafuta mtaalamu husika akusaidie
Vitu vya msingi kuwepo kwenye chumba cha kupikia (kitchen)
Ili twende sawa kwenye hiki chumba kuna maeneo matatu (3) ya msingi kuzingatiwa. Mwisho utaona picha kwa vielelezo.
1. sehemu ya kuhifadhi(preservation & storage) – Eneo hili ni vizuri kuwa karibu na mlango wakutokea ili iwe rahisi mtu akiingia tu anaweka vitu, katika nyumba kubwa hili eneo pia hutafutiwa chumba chake. Hapa kuna vitu vifuatavyo
  • Jokofu (refrigerator)
  • makabati (shelves or cupboard)
2. Sehemu ya maandalizi na usafishaji(preparation & cleaning) – Hapa ndiyo maandalizi ya vifaa vya kupikia pamoja na malighafi za mapishi zinapoandaliwa, ni vizuri kuwa karibu na dirisha. Vitu vinavyotakiwa kuwepo;
  • Meza (table)
  • Sink
3. Sehemu ya kupikia (cooking center) – hii ndiyo sehemu ya kutayarishia chakula, vitu vinavyotakiwa kuwepo;
  • jiko la kupikia (stove or range)
  • kabati la juu (shelves)
Picha za vielelezo


USIPITWE!! Endelea kuwa nasi kwa taarifa nyingine kuhusu ujenzi.

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

Jumanne, 14 Julai 2015

VIFAA 12 VYA MSINGI KUWANAVYO FUNDI BOMBA (PLUMBER)


Habari za wakati mpendwa msomaji! katika mada hii tunataka tukupitishe kwenye mambo yahusuyo vifaa vya kiufundi. Hii ni kwa ajili ya wewe fundi unaetaka kuanza shughuli(kujitegemea), au wale watu wanaotaka kuanzisha kamradi kadogo, na pia hata kwa wale watu wanaopenda viwepo majumbani kwao kwaajili ya mambo ya dharura au kupunguza makali ya gharama za kiufundi.

VIFAA VYA MSINGI KWA MAFUNDI BOMBA(PLUMBING)
1. Koleo (tongue & groove pliers) – kazi yake ni kukaza, kulegeza na kuvuta kipande cha bomba(connector) au nati. zipo za nchi 10 na nchi 12.

2. msumeno (hacksaw) – kazi yake ni kukata vipande vya bomba na nati.

3. kinoleo (metal file) – kazi yake ni kunoa (kurudisha makali) ya mabomba ya metali.

4. Basin wrench – kazi yake ni kukaza na kulegeza nati.

5. pipe wrench – hii pia hutumika kukazia na kulegeza nati ndogo zaidi na za ukubwa tofauti.

6. Adjustable wrench – kazi yake ni kubana sehemu zinazohitajika kubana kama kwenye baadhi ya sehemu zilizoungana (connector)

7. Propane torch – hili ni dumu/kidumu kilicho na gesi, kazi yake ni kuyeyusha mabomba hasa mabomba ya kopa sehemu za kuunganishia.

8. Hand auger – kazi yake ni kusafisha sink, tube na mabomba.

9. Tubing cutter – kifaa hiki kinatumika kwa kukata kwa urahisi mabomba hasa hasa mabomba ya kopa.

10. Plunger – kazi yake ni kutoa uchafu kwenye vyoo, bafu na sink.

11. Closet auger – kazi yake ni kusafisha sehemu za ndani za mabomba sink, vyoo nk.

12. koti gumu (overall) – kazi yake ni kujikinga na moto, vitu vichafu na kuwa salama kiafya.

kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965
usiache kuweka neno hapo chini
 

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506