+255 753 066 151

ujenzielekezi04@gmail.com

Ubungo Kibangu at Kinondoni Dar-es-salaam Tanzania

Jumapili, 16 Agosti 2015

USHAURI KWA WALE WANAOTAKA KUJENGA NYUMBA KWENYE KIWANJA KILICHOPO KWENYE MUINUKO



Habari za wakati mpendwa msomaji wa makala hizi za ujenzi! Lengo letu ni kuhakikisha unaendelea kutembelea mtandao huu kwa kujifunza mambo mbalimbali ya ujenzi
Katika ujenzi kiwanja ni kipande cha eneo ambacho hutumika kwa kujenga majengo mbalimbali. viwanja hutofautiana  kutoka eneo moja hadi lingine kulingana na sura ya eneo husika kama vile bondeni, milimani na tambarare.
Katika viwanja vilivyopo kwenye maeneo yaliyoinuka hususani milimani ujenzi wake huwa tofauti katika msingi(foundation) tofauti na maeneo mengine.
Kuna vitu viwili vya kuzingatia kwa wale wanaotaka kujenga kwenye viwanja vilivyopo kwenye miinuko (slope).
1. Kujenga kwa ngazi(steps) – hii ni aina ya kujenga kwa kufuata usawa (level) ya vieneo vinavyounganisha eneo zima.


2. Kujenga kwa kuchimba/kujaza – hii ni aina ya ujenzi ambayo wajenzi huchimba/kujaza udongo kwa lengo la kusawazisha kisha kuendelea na ujenzi.

Muhimu: Unapofikiria kutengeneza ramani ya kujenga ni vyema kuzingatia hili kwa sababu unaweza kuwa na ramani nzuri lakini isijengeke kwenye kiwanja chako.

Kujifunza zaidi kuhusu viwanja bonyeza maandishi ya blue hapo chini



USIPITWE!! Endelea kuwa nasi kwa taarifa nyingine kuhusu ujenzi.
kwa ushauri/maoni/swali wasiliana nasi kupitia
Namba ya simu: +255 753 066 151, +255 655 699 342, +255 714 835 965

1 COMMENT

Unknown alisema ...
26 Novemba 2019, 03:30

Naomba kupata mwongozo najua kuchora raman kwenye karatasi lakini sijui kuchora kwenye computer .idea ninayo lakini sijui nianzie wapi ?


Chapisha Maoni

Popular

All Rights Reserved UJENZI ELEKEZI | Mtengenezaji wa BLOGG CHIKULO +255657103506 | +255753103506